Monday, April 1, 2013

WALIOFARIKI WAFIKIA 34 MTAA WA INDIRA GANDHI DAR


Idadi ya waliokufa kutokana na kuporomoka kwa jengo jijini Dar es Salaam, Tanzania, imefikia 34 asubuhi ya leo, kwa mujibu wa taarifa ya serikali.

http://vml1.s3.amazonaws.com/wp-content/uploads/2013/03/Tanzania.jpgBaada ya siku tatu za kuwatafuta manusura, inaripotiwa kuwa wafanyakazi wa huduma ya uokozi hawana tena matumaini ya kuwapata watu wengine walio hai. Jengo hilo la ghorofa 16 lililokuwa likijengwa katikati ya mji huo mkubwa kabisa nchini Tanzania liliporomoka siku ya Ijumaa, ambapo ni watu 17 tu waliopatikana wakiwa hai siku hiyo. Wengi wa waliokufa walikuwa vibarua na wapita njia. Wamo pia watoto waliokuwa wakicheza mpira karibu na jengo hilo. Mashahidi wanasema kwamba kuna vibarua wengi ambao hadi sasa hawajaonekana. Katika miaka ya karibuni, kuporomoka kwa majengo kumekuwa jambo la kawaida katika nchi za Afrika ya Mashariki, ambako wamiliki wa majengo hukwepa kanuni za ujenzi kwa lengo la kupunguza gharama.

PICHA MBALIMBALI ZA AJALI YA KUFUNIKWA NA KIFUSI JIJI ARUSHA


ajali (66)Mwili wa dereva wa lori moja kubwa lenye ujazo wa tani 18 ukiwa umeopolewa na askari jeshi, tayari kupelekwa mochwari ya Hospitali ya Mt Meru. Dereva huyu ametambulika kwa jina moja tu la Alex amefikwa na mauti akiwa  ndani ya gari hilo wakati vijana wengine wakiendelea kupakia moram  asubuhi ya leo

ajali (55)Mbunge wa Arusha Mjini, Mh Godbless Lema akiwasili eneo la ajali mapema asubuhi.
ajali (44)Baadhi ya wananchi waliojitokeza kushuhudia ajali hiyo mbaya wakishangaa zoezi la uokoaji na wengine wakisubiri kutambua ndugu zao, jambo ambalo  halikupata nafasi.
ajali (65)Mwananchi huyu aliishiwa nguvu baada ya kushuhudia mwili wa rafiki yake ukiopolewa kutoka kwenye kifusi
ajali (49)Hali ilivyo machimboni hapo
ajali (64)Kina mama wakilia kwa uchungu wakihofia kuondokewa na wapendwa wao
ajali (21)Vikosi vya Jeshi la Wananchi na Polisi vikiwa kazini
ajali (35)Sehemu ndogo ya Fuso ikionekana huku gari nyingine ikiwa haionekani kabisa.
________________________________________________________________________________

Inakadiliwa watu zaidi ya watu 18 wamepoteza maisha kufuatia  kufukiwa na gema la mchanga/moram wakati wakichimba na kupakia kwenye  malori eneo la Moshono jijini Arusha.
Ajali hiyo mbaya imetokea katika machimbo ya moram nje kidogo ya jiji eneo jirani na Moshono-Kiserian ambapo vijana hao  wanaokadiriwa kufikia idadi hiyo walikuwa wakipakia moram kwenye magari mawili, moja ni Fuso na lingine kubwa zaidi (tani 18) na yote mawili yamefukiwa kabisa na kifusi. 
Shuhuda mmoja wa ajali ambae pia ni  mchimbaji ameieleza Blog hii kwamba kwa kawaida gari ndogo kama Fuso  hupakiwa na watu 7, na hiyo kubwa huwa na watu 12 bila kuhesabu dereva na utingo. 
Miongoni wa waliofikwa na mauti ni pamoja na madereva wa magari hayo. Katika eneo la ajali hali ni ya simanzi na vilio toka kwa kina mama huku baadhi wa wababa na marafiki na ndugu wa jamaa waliofukiwa wakishindwa kujizuia na kuangua kilio. 
 
Meya wa  Manispaa Mh Gaudence Lyimo pamoja na Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless  Lema ni miongoni mwa viongozi wakubwa waliofika eneo la ajali kusaidiana na kikosi cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania kufanya uokozi. 
 
Wachina wakipeleka moja ya mashine zao (Excavator) kuongeza nguvu katika kusaidia kufukua miili ya watu hao iliyonaswa na kifusi hicho.

Chanzo:
Picha/habari  
ARUSHA255 BLOG

Sunday, March 31, 2013

PAPA FRANCIS NA KADHIA YA SYRIA NA PENISULA YA KOREA


Papa Francis ameomba kufikiwa kwa ufumbuzi wa kisiasa nchini Syria na usuluhishi katika rasi ya Korea katika ujumbe wake wa kwanza wa Jumapili ya Pasaka mbele ya umati uliofurika katika uwanja wa Mtakatifu Petro. 

 http://news.bbcimg.co.uk/media/images/66684000/jpg/_66684489_francgetty.jpg
Papa huyo wa kwanza kutoka Amerika Kusini pia amesihi kuachiliwa kwa mateka wanaoshikiliwa na wanamgambo nchini Nigeria na kulaani usafirishaji haramu wa binaadamu kuwa ni aina ya utumwa wa hali ya juu katika karne hii ya 21. Papa ametowa baraka zake za kwanza za "Urbi et Orbi" kwa kuibariki Roma na dunia kwa jumla akiwa katika roshani ya Kanisa la Mtakatifu Petro ambapo alijitokeza mara ya kwanza kufuatia kuchaguliwa kwake kuwa papa mwezi huu.

WANAJESHI 5 WAFA AFRIKA KUSINI


Wanajeshi watano wa Afrika Kusini wameuawa wakati helikopta yao ilipoanguka katika doria ya operesheni ya kupiga vita ujangili. 

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02519/Solly-Shoke_2519437b.jpg 
Kwa mujibu wa taarifa ya kijeshi ajali hiyo ilitokea jana jioni katika Mbuga ya Taifa ya Kruger na uchunguzi tayari umeanza kubaini chanzo cha ajali hiyo. Afrika Kusini iko katika harakati za kukomesha uwindaji haramu wa vifaru ambapo pembe zao huuzwa kwa thamani kubwa barani Asia. Idadi ya vifaru waliouwawa nchini Afrika Kusini kuanzia mwaka huu imefikia 188 wakiwemo vifaru 135 kutoka Mbuga ya Kruger.

WANYARWANDA WAKAMATWA WAKIENDESHA UKAHABA, WAKUTWA NA ARVS


WANAWAKE watatu raia wa Rwanda wanaosadikiwa kuendesha biashara ya ukahaba mjini Dodoma wamekamatwa na kupewa siku tatu kuondoka nchini, huku wawili kati yao wakikutwa na vidonge vya kupunguza makali ya virusi ya Ukimwi (ARVs).
http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2012/12/Hussein-Mwinyi.jpg

Kukamatwa kwa wanawake hao ambao ni Esperance Hagenimana (28), Vestina Zaninika (27) na Ziada Mukamurera (25), kunafuatia mmoja wao Esperance kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi kuwa alikuwa ameibiwa fedha taslimu Sh 800,000 na hati ya kusafiria.

Lakini, Polisi walipofika nyumba ya kulala wageni waliyofikia iliyopo eneo la Area D walikuta wanawake wengine wawili ambao walikuwa wakikaa chumba kimoja na Esperance.

Uchunguzi wa Polisi ulibaini kuwa mwanamke huyo hakuibiwa na kubaini wote si raia wa Tanzania. Hata hivyo kilikosekana kifungu cha kuwashitaki ndipo waliamua kupeleka sakata hilo Uhamiaji ili liweze kushughulikiwa.

Kulingana na maelezo yao, Esperance alitangulia kuja nchini kisha kuwaita wenzake ambao ilikuwa ni mara ya kwanza kuja nchini, lakini hata hivyo alisema kuwa, kumekuwa na makundi ya wanawake kutoka Rwanda wanaokuja nchini kipindi cha Bunge na hata mwaka jana kuna kundi lilikuja wakati wa mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kulingana na uchunguzi uliofanywa na Uhamiaji, wanawake hao waliingia nchini na kujitambulisha kuwa walikuja Dodoma kufanya biashara ya vitenge, lakini hawakuwa hata na kitenge kimoja ambacho kingeweza kuwaonesha kuwa walikuwa wakifanya biashara hiyo.

Juhudi hizo za Uhamiaji zinadaiwa kuwafikisha hadi klabu moja maarufu ya usiku iliyopo eneo la Area D ambapo walinzi wa Kimasai walikiri kuwafahamu wanawake hao na walikuwa wakiwafuata nyumba ya wageni waliyofikia kama mtu alikuwa akiwahitaji na walikuwa na ni wateja wa klabu hiyo ya usiku.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma, Norah Massawe alikiri kukamatwa kwa wanawake hao na polisi na kukabidhiwa Uhamiaji.
CHANZO: HABARILEO.

AMUINGILIA MBUZI KUOGOPA KUPATA VVU/UKIMWI

SAKATA la mkazi wa Kijiji cha Madunga,Kata ya Madunga Wilaya ya Babati Mkoani Manyara,kuwaingilia mbuzi wa eneo hilo,limechukua sura mpya baada ya mmoja kati ya mbuzi aliowaingilia kuharibika mimba.

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/d/d2/Brown_female_goat.jpgAidha mmiliki wa mbuzi huyo  wakati akiongea na waandishi wa habari Clementina Masay alisema kuwamtuhumiwa huyo ambaye amekuwa akiwabaka mbuzi na kuwaingilia kwa nguvu amemsababishia hasara baada ya mimba ya mbuzi wake jike kuharibika.

Ameongeza  kuwa Serikali inatakiwa imchukulie hatua kali mtuhumiwa huyo kwani baada ya kufikishwa Mahakamani na kufunguliwa kesi alipata dhamana lakini hadi hivi sasa ametorokea sehemu isiyofahamika.

Ameendelea kusema kuwa mtuhumiwa huyo,Daniel Marcel mwenye umri wa miaka 22 alifunguliwa kesi namba 29/2013 kwa kosa la kuiingilia mifugo,kinyume na kifungu cha 325 kanuni ya adhabu sura ya 16 na alipopata dhamana akatoroka.

Kesi hiyo ipo mbele ya Hakimu Julius Dagharo wa Mahakama ya Mwanzo Bashnet,ambaye ndiye aliyemsomea shtaka na Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho Omari Mwanditi alikiri mshtakiwa huyo kutoroka baada ya kupatiwa dhamana.

Pia jamii ya wafugaji wa kiiraq wa eneo hilo wamesikitishwa na kitendo cha mifugo yao kuingiliwa mara kwa mara kwa kunajisiwa na walidai kuwa watamsaka mtuhumiwa huyo hadi wamkamate kwani kitendo hicho kimewasikitisha.

Aidha wamesema matukio ya mtuhumiwa huyo kuwaingilia mifugo yamekuwa yakitokea mara kwa mara na pindi anapoulizwa anadai kuwa anaiingilia mifugo kwa kuogopa kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi.

15 WAFA KATIKA MAPAMBANO NA BOKO HARAM

Wanajeshi leo wameyavamia maficho ya washukiwa wa kundi la itikadi kali za Kiislamu Boko Haram katika mji mkubwa wa kaskazini mwa Nigeria Kano, na kuchochea vurugu ambazo zimesababisha vifo vya watu 15.
 
http://www.csmonitor.com/var/ezflow_site/storage/images/media/content/2012/0321-boko/12077807-1-eng-US/0321-boko_full_600.jpgJeshi limedai kuwa waliouawa walikuwa ni pamoja na wanamgambo 14 wa Kiislamu na mwanajeshi mmoja, wakati likidai kuwa wapiganaji hao walikuwa wakipanga kufanya shambulizi la siku kuu ya Pasaka mjini humo. Wakaazi wamesema wamesikia milio ya risasi wakatai majeshi yakipambana na wapiganaji. Jeshi limedai kunasa silaha, ikiwa ni pamoja na gari lililokuwa na miripuko tayari kufanya shambulio.