Monday, January 14, 2013

WAHINDU WAOGA KATIKA MTO GANGES


Wahindu katika mto Ganges
Mamilioni ya waumini wa madhehebu ya Hindu nchini India wamejitosa katika mto wao mtakatifu, Ganges, kitendo ambacho wanaamini kinawaosha dhambi zote. 
Siku ya leo inachukuliwa kama siku yenye heri kubwa zaidi katika  maadhimisho ya siku 55 yajulikanayo kama Kumbh Mela, ambacho umuhimu wake unatokana na masuala ya kinajimu. Afisa mkuu wa maadhimisho hayo Mani Prasad Mishra amesema kwamba tayari watu milioni tatu wamekwishaingia ndani ya mto Ganges kuanzia asubuhi, na kwamba wanategemea kuwa ifikapo jioni watu milioni kumi na moja watakuwa wamejiosha na maji ya mto huo yenye baridi kali. Wakereketwa wa dini ya Hindu wanaamini kwamba kuoga ndani ya mto Ganges kunaondoa dhambi zao, na kuwaepusha na mzunguko wa kifo na kuzaliwa kwa mara ya pili.

TENGA KUTOGOMBEA TENA URAIS TFF


     Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amesema hatagombea tena wadhifa huo katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Februari 24 mwaka huu.
Leodegar Tenga

Akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye ofisi za TFF leo, Rais Tenga amesema wakati anaingia kwenye uongozi mwaka 2004 ajenda ilikuwa na kuijenga TFF kama taasisi kwa kuweka mifumo ya uendeshaji ikiwemo kutengeneza katiba na kanuni, jambo ambalo limefanyika.

“Wajumbe wamekuwa wakiniuliza Rais vipi? Mimi hapana. Nilishafika pale pa kufika. Tulipoanza wakati ule ilikuwa ni kujenga taasisi. Na kazi hiyo tumeifanya. Tulipoingia mwaka 2004 hiyo ndiyo ilikuwa ajenda,” amesema Rais Tenga.

Amesema walitengeneza Katiba, vyombo huru vya kufanya uamuzi, kuongeza wigo wa wapiga kura ambapo hivi sasa kwenye mpira wa miguu hakuwezi kutokea migogoro, hata ikitokea kuna mfumo wa kuidhibiti.

Rais Tenga ameishukuru Sekretarieti ya TFF, Kamati ya Uchaguzi ya TFF, kamati za uchaguzi za wanachama wa TFF na vyama wanachama wa TFF kwa hatua iliyofikiwa katika uchaguzi ambapo mikoa yote imekamilisha uchaguzi na kubaki vyama shiriki pekee.

Ametoa mwito kwa wadau kujitokeza kugombea uongozi TFF, kwani baada ya kujenga taasisi ajenda iliyobaki ni mpira wa miguu wenyewe ikiwemo nini kifanyika ili mpira uchezwe katika maeneo mbalimbali.

“Tumeshatengeza mfumo, sasa ni kuangalia jinsi ya kuendeleza mpira. Changamoto ni tufanye nini ili mpira uendelee. Tunataka watu wengine wabebe hiyo ajenda ili tuangalie tunakwendaje mbele,” amesema.

Pia amesema ushirikiano ambao amepata kwa wapenzi na wadau wa mpira wa miguu ni wa ajabu. Vilevile ameishukuru vyombo vya habari, Serikali, klabu, wadhamini na wafadhili kwa mchango wao katika uendeshaji wa mpira wa miguu nchini.

19 WACHUKUA FOMU UCHAGUZI TFF


Wadau 19 wamechukua fomu kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) unaotarajiwa kufanyika Februari 24 mwaka huu.
 
Fomu hizo zimeanza kutolewa leo (Januari 14 mwaka huu) ambapo wawili wamechukua nafasi ya Makamu wa Rais wakati waliobaki wanaomba ujumbe wa Kamati ya Utendaji wakiwakilisha kanda mbalimbali.

Waliochukua fomu za umakamu wa rais ni Wallace Karia na Ramadhan Nassib. Wote ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF inayomaliza muda wake.

Waliochukua fomu za ujumbe ni Shaffih Dauda, Athuman Kambi, Hussein Mwamba, Stewart Masima, Yusuph Kitumbo, Mugisha Galibona, Vedastus Lufano, Twahili Njoki, Charles Mugondo, Elley Mbise, Farid Nahdi, Ayubu Nyaulingo, Nazarius Kilungeja, Epaphra Swai, Khalid Abdallah, James Mhagama na Selemani Bandiho.

PONGEZI UONGOZI MPYA KATAVI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Katavi (KAREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Januari 13 mwaka huu).

Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa KAREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Katavi.

TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya KAREFA chini ya ukatibu wa Peter Hella aliyeibuka mshindi katika uchaguzi huo uliofanyika ukumbi wa DC mjini Mpanda kwa kumshinda Emmanuel Chaula kwa kura sita dhidi ya mbili.

Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Katavi kwa kuzingatia katiba ya KAREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.

Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya KAREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.

Viongozi waliochaguliwa ni Hella (Katibu), Elias Mande (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF) na Deo Bakuba (Mwakilishi wa Klabu TFF). Nafasi ya Mwenyekiti haikuwa na mgombea wakati Mawazo Maso aliyekuwa mgombea pekee wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti alipata kura nyingi za hapana. Nafasi zilizo wazi zitajazwa katika uchaguzi mdogo.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Sunday, January 13, 2013

VIWANJA VYA MPIRA AFRICA



NATION STADIUM
MOSES MABHIDA STADIUM
 Nelson Mandela Bay Stadium
NELSON MANDELA STADIUM
MBOMBELA STADIUM
Royal Bafokeng
ROYAL BAFOKENG

MAKUNDI YA TIMU AFRICA



Africa Cup of Nations 2013

Group A



Pos
Team
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Angola
0
0
0
0
0
0
0
0
2
Cape Verde Islands
0
0
0
0
0
0
0
0
3
Morocco
0
0
0
0
0
0
0
0
4
South Africa
0
0
0
0
0
0
0
0

Group B



Pos
Team
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Congo DR
0
0
0
0
0
0
0
0
2
Ghana
0
0
0
0
0
0
0
0
3
Mali
0
0
0
0
0
0
0
0
4
Niger
0
0
0
0
0
0
0
0

Group C



Pos
Team
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Burkina Faso
0
0
0
0
0
0
0
0
2
Ethiopia
0
0
0
0
0
0
0
0
3
Nigeria
0
0
0
0
0
0
0
0
4
Zambia
0
0
0
0
0
0
0
0

Group D



Pos
Team
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Algeria
0
0
0
0
0
0
0
0
2
Ivory Coast
0
0
0
0
0
0
0
0
3
Togo
0
0
0
0
0
0
0
0
4
Tunisia
0
0
0
0
0
0
0
0

BOZIZE AVUNJA BARAZA LA MAWAZIRI


Amri ya rais iliyosomwa kupitia televisheni ya taifa, ilifuta amri nyingine ya Aprili 22, 2011,inayohusiana na uteuzi wa serikali. Chini ya makubaliano ya amani, serikali mpya itaongozwa na mjumbe wa kisiasa kutoka upinzani, na kuandaa uchaguzi wa wabunge ndani ya miezi 12 kuchukua nafasi ya bunge la sasa linalodhibitiwa na washirika wa Bozize. 

Makundi matano yanayounda muungano wa Seleka yalikubali kusitisha mapigano kufuatia makubaliano hayo, na hivyo kukomesha kitisho kikubwa zaidi kwa utawala wa muongo mmoja wa Bozize.