Monday, April 22, 2013

WATU 185 WAFA NIGERIA KUTOKANA MAPIGANO BAINA YA BOKO HARAM NA JESHI LA NCHI HIYO


Watu wasiopungua 185 wameuliwa kaskazini mashariki mwa Nigeria katika mapigano kati ya vikosi vya jeshi la nchi hiyo na wapiganaji wa Boko Haram. 

 http://serving.thisdaylive.com/0bef99d6-acf5-4e2c-9779-8fa02ba3fcd4/assets/Boko-Haram-Suspects.jpg?maxwidth=400&maxheight=540
Lewa Kole afisa wa serikali za mitaa amemueleza gavana wa jimbo la Borno Kashin Shettima kuwa mapigano yalianza Ijumaa iliyopita huko Baga katika jimbo la Borno na kudumu kwa masaa kadhaa.

Hata hivyo bado haijafahamika ni askari, raia au wanamgambo wangapi wa Boko Haram waliouliwa katika mapigano hayo kwa kuzingatia kuchomwa moto viwiliwili vingi ambavyo havijaweza kutambuliwa, kufuatia moto ulioteketeza karibu mji huo wote. Brigedia Jenerali Austin Edokpaye amesema kuwa raia wengi walitumiwa na wapiganaji wa Boko Haram kama ngao ya binadamu katika mapigano hayo.

Tuesday, April 16, 2013

LAIZER AWATAKA WAFUGAJI WA KIMASAI KUPUNGUZA MIFUGO KWA KUUZA

Mbunge wa Jimbo la Longido Michael Lekule Laizer kwa titketi ya Chama cha Mapinduzi amewataka wafugaji wa kimasai katika Jimbo lake kupunguza mifugo hiyo kwa kuiuza ili kuongeza mapato yatokanayo na mifugo yao.

Katika mahojiano mapema leo asubuhi Mheshimiwa Lekule Laizer amesema endapo wafugaji wa kimasai watatambua kuwa mifugo waliyonayo ni rasimali tosha ya wao kukua kiuchumi basi itasaidia jimbo lake kuwa katika hali nzuri.

Laizer amesema kwa muda mrefu sasa kauli mbiu ya kupunguza mifugo imeonekana kutozaa matunda kutokana na mila na desturi za kimasai kutotaka kupunguza mifugo hiyo.

Pia ameongeza kusema kwa sasa kuna mabadiliko ya tabia nchi ambapo yamefanya hata mifugo kutoweza kufugika kwani hata katika jimbo lale kulitokea maafa ya ng’ombe kufa kutokana na misimu mitatu ya mvua kutonyesha katika ardhi yao.

Laizer amesema endapo watauza mifugo hiyo watatakiwa kuweka fedha zao benki kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikwemo kujenga nyumba, kusomesha watoto.

Aidha Mbunge huyo amesema tangu mwaka 1995 alipoingia madaraka kulisimamia jimbo hilo amewatendea wananchi mahitaji muhimu huku akitajihidi kupitia serikali ya CCM iliyopo madaraka kukamilisha ahadi zake kwa wananchi.

BOSTON MARATHON ZA SABABISHA VIFO MAREKANI


Mpaka sasa watu watatu wameshakufa kutokana na mashambulio ya mabomu mawili yaliyoripuka wakati wa mbio ndefu za marathon katika mji wa Boston nchini Marekani. 

Mashambulio ya mabomu, BostonMabomu mawili yaliripuka kwenye mitaa iliyokuwa imejaa watu karibu na sehemu ya kumalizia mbio za marathon. Watu wasiopungua watatu wamekufa kutokana na miripuko ya mabomu hayo yaliyoutikisa mji wa Boston katika jimbo la Marekani la Massachusettes.

Je ni magaidi tena?
Watu wengine zaidi ya140 walijeruhiwa katika kadhia ya umwagikaji wa damu. Vioo vilivunjika na sehemu za miili ya binadamu ilitapakaa- hali iliyosababisha wasiwasi kwamba magaidi wameishambulia tena Marekani. Msemaji wa Ikulu ya Marekani ambae hakutaka kutajwa kwa sababu uchunguzi bado unaendelea, ameeleza kuwa mashambulio hayo yanazingatiwa kuwa ni kazi ya magaidi.

Akitoa tamko juu ya mashambulio hayo Rais Obama aliepuka kutumia neno gaidi, alieleza kwamba maafisa wa Marekani hawajui ni nani aliyeyatega mabomu hayo na kwa nini. Hata hivyo afisa mmoja wa Ikulu ya Marekani alisema baadae kuwa miripuko hiyo iliyotokea kwenye mbio za marathoni zenye jadi ya miaka mingi, inazingatiwa kuwa kitendo cha ugaidi.

Obama asema aliefanya mashambulio atapatikana:
Rais Obama alilihutubia taifa kwa kuwahakikishia Wamarekani kwamba, tukio hilo litachunguzwa kwa undani. Obama alisema "Tutabainisha nani ameyafanya mashambulio haya na kwa sababu gani." Ameeleza kuwa wote wale waliohusika, au kikundi chochote- kitauona mkono mkali wa sheria. Rais Obama amesema Marekani itamjua alieyafanya mashambulio hayo.

Mabomu hayo mawili yalipishana kwa muda wa sekunde chache tu. Mwokoaji anaetoa huduma ya kwanza, amesema wanajaribu kupata damu kwa haraka. Amearifu kuwa wapo waliojeruhiwa kwa kukatika viungo vya mwili na, wengine waliumizwa na vipande vya vioo, na pote palisambaa damu.

CHANZO: DW/DPA

Monday, April 8, 2013

TFF YATAKA MAELEZO YA MCHEZAJI KUHUSU RUSHWA


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemtaka mshambuliaji Nsa Job wa Coastal Union kuwasilisha maelezo yake juu ya madai kuwa alipewa rushwa ya sh. milioni mbili ili asiifunge moja ya timu vigogo vya soka nchini.

http://2.bp.blogspot.com/-PPp2IXpaP5Y/Txk52BJmw9I/AAAAAAAAETQ/DDznTiZJz4Y/s400/tff+LOGO.jpg
Job alikaririwa Aprili 3 mwaka huu na kituo cha redio cha Clouds FM katika kipindi cha Amplifier kuwa alipewa kiasi hicho cha fedha na kiongozi wa timu husika ili asiifunge katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom, lakini alipokea fedha hizo na kuifunga timu hiyo.

Baadaye kiongozi huyo alikuwa akimtaka arejeshe fedha hizo. Pia TFF imekiandikia kituo hicho cha redio kutaka nakala ya kipindi hicho ili pamoja na maelezo ya mshambuliaji huyo vipelekwe katika Kamati ya Nidhamu kwa ajili ya hatua za kinidhamu.

TFF itachukua hatua kali dhidi ya Job iwapo hatawasilisha maelezo yake kuhusiana na suala hilo, na imetaka wadau kutoa ushirikiano ili iweze kupambana kikamilifu na vitendo vya rushwa kwenye mpira wa miguu.
  
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

SAMOA AIR KUTOZA NAULI KULINGANA NA UZITO

Shirika la ndege la Samoa Air katika visiwa vya Samoa, limeanza kutoza nauli ya abiria wake kutokana na uzito walio nao. Hatua hiyo imeibua hisia tofauti miongoni mwa wasafiri wa ndege kisiwani humo.

Tatizo la kuongezeka kwa unene na uzito wa watu duniani, limekuwa likiangaliwa kama ni moja ya hali inayosababisha harasa kubwa kwa jamii. Lakini hivi karibuni, katika visiwa vya Samoa, kumegunduliwa njia mbadala ambayo inaleta tija kwa jamii husika, na kutoa ujumbe ya kuwa ukiwa mnene na mzito kupita kiasi, basi kuna faida utakayoleta katika kukuza biashara ya usafiri, hususan katika swala la kutumia usafiri wa anga au ndege kama chombo cha kusafiria.

Hivyo wakazi, wanachi na wageni ambao watasafiri kutumia usafiri wa shirika la ndege la Samoa watakuwa wakipimwa uzito wao, ili kuweza kujua ni kiasi gani watalipa kutegemea na umbali wa eneo watakalosafiri ndani ya visiwa hivyo.

Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2011 za shirika la afya ulimwenguni, WHO, asilimia 86% ya wananchi wa Samoa wanakabiliwa na tatizo la unene na hivyo kushika nafasi ya nne duniani kwa kuwa na watu wenye uzito na unene kulinganishwa na Marekani yenye asilimia 69% Australia 61% na Japan 22%.
Akitetea uamuzi huo wa shirika la ndege la Samoa Air kuwalipisha nauli abiria kutokana na uzito walionao, Chris Langton, ambaye ni mkurugenzi wa shirika hilo alisema, "hii ni haki kwani mashirika ya ndege, yamekuwa yakisita kufanya hiyo kwa kuhofia hali ya utu wa mtu, lakini gharama za usafiri zimekuwa zikitozwa kutokana na uzito, kwani gharama za uendeshaji wa usafari wa anga umekuwa ukilipiwa kutokana na uzito siyo nafasi za viti, na abiria wetu wamekuwa wakipimwa uzito kabla ya kusafiri, japokuwa wengi wao wamekuwa wakishangaa lakini hawalipingi jambo hilo."

Akiongezea katika swala zima la kutozwa nauli huko, Langton alisema "ikiwa abiria anataka nafasi zaidi atapewa kulingana na matakwa yake, na tunahakikisha kuwa hakutokei makosa katika upimaji huo, kwani si halali kwa mtoto wa miaka 12 na 13 ambaye ana uzito mdogo kulipa nauli ya mtu mzima badala ya kulipa kutokana na uzito wake.

Abiria walalamika
Ana Fapouli abiria na ambaye ni raia wa visiwa hivyo na anayesafiri mara kwa mara kutumia usafiri huo, amesema " kupandishwa kwa nauli kutokana na uzito wa abiria kutanufaisha shirika hilo la Samoa Air kwani wameona njia ya kuongeza faida, na watakuwa na mashindano ya kibiashara na mashirika mengine mawili yanaoyotoa huduma ya usafiri wa anga kwa abiria wa wanaoingia na kutoka Samoa."

Naye mkurugenzi mkuu wa afya wa Samoa, Palanitina Toelupe, akilizungumzia swala hili la abiria kulipa naili kulingana na uzito wao alisema "mpango huu unaweza kuwa mzuri wa kuhamasisha watu kupunguza uzito na kuwafanya wawe wanakula vyakula vyenye afya na unaleta maana, lakini kwa upande mwingine, usafiri wa anga utakuwa ghali kwa watu walio na maumbile ya unene na wazito, jambo ambalo tutalijadili tutakapokutana na viongozi wa shirika na pia nafikiria kuwa ni sehemu ndogo ya ujumbe kwa watu wapunguze uzito na unene."
Hata hivyo swala zima la kutozwa nauli kubwa kutokana na uzito wa abiria, limekuwa likiendelea tangu mwezi Novemba mwaka jana, baada ya kupewa baraka na idara ya usafiri ya Marekani, wakati lilipopitisha muswada wa kulipishwa nauli kutokana na uzito wa abiria, kwa wasafiri wote waendao visiwa vya Samoa.

Uamuzi huo wa shirika la ndege la Samoa wa kulipisha nauli kutokana na uzito wa mtu huenda ukaigwa na mashirika mengine ya ndege siku zijazo, ili kukuza kampeni ya kupunguza uzito na unene.

Mwandishi. Rukundo Laurance/APE/AFPE
Mhariri. Josephat Charo, DW

JKT RUVU YAPANIA KUBAKIBAKI LIGI KUU


Mchezaji nguli wa maafande wa JKT Ruvu, pia aliyewahi kutamba akiwa na wekundu wa Msimbazi Simba, DC Mote Mapembe ya jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo pamoja na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa stars, Musa Hassan Mgosi ametamba kuiokoa klabu yake isishuke daraja msimu huu.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na matandao huu, Mgosi ambaye jina lake ni la kibantu likimaanisha mwanaume, amesema kamwe timu yake haiwezi kushuka daraja kufuatia hali yake kuimarika na kurudi katika kiwango chake cha kawaida.

Nyota huyo ambaye jina lake haliwezi kusahaulika kwa wana Msimbazi kutokana na kufunga magoli muhimu, aliongeza kuwa ligi ya sasa ina ushindani mkubwa sana huku kila timu inaonekana kuwa imara zaidi inapocheza mechi.
http://www.footballzz.com/img/jogadores/66/56966_ori_musa_mgosi.jpgphilelyk.blogspot.comMgosi aliongeza kuwa yeye ni mchezaji wa kimataifa na ana uzoefu mkubwa wa kufunga magoli, hivyo lazima aibebe JKT Ruvu msimu huu ikiwa ni sehemu ya kuilipa fadhila timu hiyo aliyoanza nayo katika safari yake ya soka.

Akizungumzia ndoto zake za kurudi timu ya taifa kwa mara nyingine, Mgosi alisema yeye ni mchezaji mwenye imani mkubwa na nidhamu kubwa ya mazoezi, hivyo ataweza kurudi tena timu ya taifa inayonolewa na kocha Kim Paulsen.

Mgosi alisisitiza kuwa timu ya taifa ya sasa ina wachezaji wazuri, wanapata huduma zote kutoka kwa wadhamini, hivyo anatamani kurudi ili alitumikie taifa kwa moyo wote.

Maafande wa JKT Ruvu wapo hatarini kuaga michuano ya ligi kuu, kwani mpaka sasa wamejikusanyia pointi 22 wakiwa nafasi ya 10 kati ya timu 14 za ligi hiyo.

Jumatano ya Aprili 10 watakuwa ugenini katika dimba la CCM Mkwakwani Mkoani Tanga “waja leo waondoka leo” kumenyana na wagosi wa kaya Coastal union.

Sunday, April 7, 2013

TUSIMSAHAU STEVEN KANUMBA (THE GREAT KANUMBA): Zitazame picha zake mbalimbali wakati wa uhai wake.


Habari za msiba wake zilianza kuenea na kusambaa kama moto wa nyika usiku wa Ijumaa tarehe 7 mwaka 2012.Kila aliyepata taarifa hakuamini. Ilikuwa ni kama ndoto au jinamizi tu ambalo baada ya muda litapita na kila kitu kitakuwa sawa.
Kulipokucha,taarifa ambazo zilianza kama uvumi na kutoaminiwa na wengi, zikaanza kuthibitishwa na watu mbalimbali hususani waliokuwa naye karibu usiku ule.Uvumi ukawa ukweli. Steven Charles Kanumba akawa ameiaga dunia tarehe 7 April, 2012 akiwa na umri mdogo tu wa miaka 28 (Steven alizaliwa tarehe 8 Januari mwaka 1984 mkoani Shinyanga) .Kifo chake kikaacha huzuni na majonzi makubwa hususani kwa mashabiki wake na wa filamu ndani na nje ya Tanzania wakiwa hawaamini na kulia kwa uchungu usio kifani.