Wednesday, December 26, 2012

FATHER AMBROS APIGWA RISASI - ZANZIBAR


        Watu wasiojulikana jana wamempiga risasi Father, Ambros Mkenda wa Kanisa Katoliki la Mpendae Mjini Zanzibar nje ya nyumba yake majira ya saa 12 jioni wakati akitokea kanisani.                                                                                                                                                    
Father Ambros Mkenda
      Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Aziz Juma Mohammed amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo alisema Father amepigwa risasi na ameumizwa sehemu ya kichwa na amekuwa akitoka damu nyingi kichwani na tayari anapatiwa matibabu katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja.                                                                                                              
           Amesema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini wahusika walifanya uhalifu huo kwa madhumuni gani kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria.                                        
     Kamanda Aziz akisimulia tukio hilo alisema walipata taarifa majira ya saa 2 na kwenda katika eneo la tukio ambapo Father alikuwa akitokea kanisani na kutaka kuelekea nyumbani kwake wakati akiwa ndani ya gari ndipo aliposhambuliwa na watu wasiojulikana na kuanguka.                                                            
       Aidha Kamanda Azizi amesema Father Ambros yeye ni mhasibu pale kanisani na hivyo mara nyingi watu wananaamini kwamba katika siku za krismass mara nyingi sadaka hukusanywa fedha nyingi na hivyo wanamini kwamba alikuwa fedha mikononi na ndipo inawezekana waliamua kumpiga risasi wakitaka kuchukua fedha hizo.                                                                 
     Hata hivyo amesema uchunguzi wa awali ndio utakaoeleza ni suala gani lililopelekea kupigwa risasi lakini wanaendelea na uchunguzi huo ambapo uchunguzi ndio utakaojulikana sababu kamili ya tukio hilo.                                                                                                                                 
     Akizungumzia tukio hilo, Askofu Michael Hafidh wa Kanisa la Anglikan la Mkunazini amesema wamesikitishwa na wamepokea kwa mshituko mkubwa tukio hilo hasa kwa kuzingatia matukio kama hayo hayajawahi kutokea ya kuwahujumu viongozi wa dini.                     
CHANZO: ZANZIBAR YETU

Monday, December 24, 2012

RAIS WA TANZANIA ATOA MILIONI 30 KWA MRADI WA KULEA NA KUHIFADHI MBWA MWITU HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI MKOANI MARA

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania akikata utepe
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wa Tanapa Jumapili Desemba 22, 2012 atoa mchango wa milioni 30 ili kuzindua boma maalumu la kulea na kuhifadhi mbwa mwitu kuashiria rasmi kuachiwa huru kundi la pili la wanyama hao (15) waliokuwa wamehifadhiwa kwa miezi kadhaa kwenye boma maalumu la mradi huo, lililojengwa katika eneo la Nyamuma, Magharibi mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, mkoani Mara.

MECHI YA TANZANIA STARS VS CHIPOLOPOLO YAINGIZA MIL 109/-

  Pambano la kirafiki la kimataifa kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Zambia (Chipolopolo) lililochezwa juzi (Desemba 22 mwaka huu) limeingiza sh. 109,197,000. Fedha hizo zimepatikana kutokana na watazamaji 17,383 waliokata tiketi kushuhudia mechi kwa kiingilio cha sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.                                                                                             
    Mgawanyo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ni sh. 16,657,169.49, maandalizi ya mchezo sh. 55,339,510, tiketi sh. 5,803,900, ulinzi na usafi kwa Uwanja wa Taifa sh. 2,350,000, Wachina (technical support) sh. 2,000,000, umeme sh. 300,000 na maandalizi ya uwanja (pitch marking) sh. 400,000.                                                                                                                                
    Nyingine ni bonasi kwa Taifa Stars sh. 13,826,313, asilimia 20 ya gharama za mchezo sh. 2,504,022, asilimia 10 ya uwanja sh. 1,252,011, asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 626,005 na asilimia 65 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 8,138,070.   
    Mapato ya mechi nyingine za Taifa Stars ilizocheza nyumbani mwaka huu yalikuwa Taifa Stars vs Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC (Leopards) iliyofanyika Februari 23 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam sh. 32,229,000. Taifa Stars vs Msumbiji (Mambas) iliyochezwa Februari 29 mwaka huu sh. 64,714,000.                                                                                                    

    Taifa Stars vs Malawi (The Flames) iliyochezwa Mei 26 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam iliingiza sh. 40,980,000. Taifa Stars vs Gambia (The Scorpions) iliyochezwa Juni 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam zilipatikana sh. 124,038,000 na Taifa Stars vs Kenya (Harambee Stars) iliyofanyika Novemba 14 mwaka huu Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza iliingiza sh. milioni 45.                                                                                                                                

Friday, December 21, 2012

Mheshimiwa Godbless Lema awa tena mbunge wa Arusha

Mheshimiwa Godbless Lema



Mahakama ya Rufaa imempa ushindi Mbunge wa Arusha mjini Mh. Godless Lema

(CHADEMA), 

aliyekuwa amefungua kesi ya kupinga maamuzi ya Mahakama Kuu ya Arusha iliyokua 

imefuta 

Ubunge wake wa Jimbo la Arusha mjini.

Thursday, December 20, 2012

Real Madrid na Man United Nani zaidi katika kinyanganyiro kijacho?

Hivi kati ya Real Madrid na Man U kukutana UEFA mnaichukuliaje? Nani ana nafasi ya kushinda?

Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi Atangaza Matokeo ya Darasa la Saba 2012


Waziri wa Elimu na  Mafunzo ya Elimu Dr. Shukuru Kawambwa

  WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa leo ametangaza matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2012 uliofanyika nchini kote  tarehe 19 na 20 Septemba, 2012.   

   Katika Mtihani huo Jumla ya wanafunzi 894,881 walisajiliwa kufanya mtihani huo ambapo   wavulana ni  426,285 sawa na asilimia 47.64  na wasichana ni 468,596  sawa na asilimia 52.36. Aidha, kati ya  wanafunzi hao, wapo wanafunzi 874,379  ambao walitarajiwa kufanya mtihani huo kwa lugha ya Kiswahili na wanafunzi 20,502 walitarajiwa kufanya kwa lugha ya Kiingereza ambayo ndiyo waliyoitumia kujifunzia.  

  Wanafunzi wasioona waliosajiliwa kufanya mtihani ni 92 wakiwemo wavulana 53 na wasichana 39.  Watahiniwa wenye uono hafifu ambao huhitaji maandishi makubwa ni 495, kati yao wavulana ni 238 na wasichana ni 257.

Wednesday, December 19, 2012

A Touching Story

  There was a man whose wife
was pregnant, One day they
were eating, along the line the
woman fell down and died, the
woman was rushed immediately
to the hospital to know if the
baby in her womb was still alive,
when they arrived the hospital,
they rushed her into the
operation room, the doctor
quickly operated on her, and the
baby was brought out alive, The
husband of the woman started
praying to God, with tears rolling
out from his eyes, telling God to
make her wife to be alive, since
the baby came out alive,
immediately the doctor finish
operating on the woman, Behold
the woman was found
breathing, everybody in the
hospital both the husband were
shocked and they begin to
thank God for such a Miracle.

    Now listen carefully!
I decree by the name that is
above all other names, let there
be peace to every storms you are
facing, anything that seems
impossible in your life, shall be
possible beginning from today,
kings shall come to your rising,
no more delay again in your life,
beginning from today you shall
experience supernatural speed
in whatever you tend to achieve
in life.
***So shall it be in Jesus name!***
       ***Phile Lyk***
 http://facebook.com/pshayo2