
Akizungumza na paparazi wetu Jumanne ya wiki iliyopita, Kinondoni Makaburini, jijini Dar, Richie alikiri kupokea simu nyingi za kina dada tangu siku ile ya uzinduzi wa filamu ya Lulu, Foolish Age uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City wakimuomba urafiki wa kawaida kumbe wana yao moyoni.
“Duh! Umeipata! Ni kweli kabisa simu ni nyingi siku ile tulikutana na mashabiki wetu wengi sana, wakachukua namba lakini kumbe wengi wao lengo lilikuwa ni kutaka mkwanja, daah Napata usumbufu kweli kwa kupigiwa simu kila dakika,” alisema Richie.
No comments:
Post a Comment