Sayari hiyo iliyopewa jina la 2012 DA 14 ina kipenyo cha mita 68, na uzito wa tani laki nne itapita karibu na dunia saa nne na dakika ishirini na tano kwa saa za Afrika Mashariki, hii ikiwa ni kwa mujibu wa shirika la anga la Ulaya, ESA.
Friday, February 15, 2013
SAYARI MPYA (2012 DA 14) KUPITA KARIBU NA DUNIA LEO USIKU
Usiku wa leo, sayari ndogo itaikosakosa dunia kwa umbali wa kilomita 27,000.
Thursday, February 14, 2013
Monday, February 11, 2013
BREAKING NEWS
Habari zilizopo ni kuwa leo Geita mapigano yametokea kati ya Waislamu na Wakristo (particular Protestants wa AIC). Na hii ni baada ya Wachungaji wa AIC kutenga eneo la Buselesele kwa ajili ya machinjio ya Wakristo wao,maeneo ya Katoro na jirani ni vurugu na mtifuano!
ASKOFU MSARIKIE KUZIKWA FEB 14 MOSHI
Askofu Mstaafu Amedeus Msarikie wa Jimbo Katoliki Moshi, aliyefariki dunia hivi karibuni, anatarajiwa kuzikwa kwenye Kanisa kuu la Kristu Mfalme, Jimbo Katoliki Moshi, hapo tarehe 14 Februari 2013.
Sunday, February 10, 2013
NECTA-MATOKEO YA KIDATO CHA NNE BADO

Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limesema matokeo ya kidato cha nne bado hayajakamilika na kuwa habari zilizozagaa wiki hii kuwa yapo tayari si za kweli.
Hata hivyo Baraza hilo limebainisha kuwa licha ya kutokamilika, matokeo hayo yanakaribia kutoka kwa mujibu wa ratiba za baraza hilo ambapo hutakiwa kutoa matokeo hayo mwezi Februari.
Akizungumza na mwandishi jana, Ofisa Habari na Mawasiliano wa NECTA, John Nchimbi alisema uvumi wa kwamba matokeo hayo yako tayari ulitokana na kuzushwa kupitia mtandao wa kijamii (Facebook).
Alifafanua kwamba habari kuwa matokeo hayo yameanza kutoka kisirisiri kabla hayajatangazwa rasmi na kwamba hatua hiyo inalenga kuyachakachua, siyo taarifa sahihi.
Aliwataka wananchi kuwa makini na uvumi huo kwa vile endapo matokeo hayo yatakuwa tayari yatatangazwa na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo na pia kuwekwa kwenye tovuti ya Baraza pamoja na wananchi kuweza kuyapata kupitia simu zao za mkononi.
Aliwataka wananchi kuwa makini na uvumi huo kwa vile endapo matokeo hayo yatakuwa tayari yatatangazwa na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo na pia kuwekwa kwenye tovuti ya Baraza pamoja na wananchi kuweza kuyapata kupitia simu zao za mkononi.
Saturday, February 9, 2013
HAWA NDIO BINADAM WALIVYO
1. Wakikukwepa usijali. Ipo siku watakutafuta.
2. Wakikusengenya nyamaza. Huenda watanyamaza.
3. Wakikununia omba Mungu. Ipo siku Watakuchekea.
4. Wakikupongeza uswaamini saana. Labla wanakukashifu!
5. Wakikutenga achana nao kwakua hawana MBINGU ya kukuweka na wao sio kila kitu.
6. Wakikudhulumu. Shukuru Mungu atakulipa marambili zaidi.
7. Wakikualika kuamakini. Isiwe wanakutega tuu.
HATA YESU ALIPENDWA HIVYO MPAKA AKASULUBIWA MSALABANI NA SASA YU HAI AMEFUFUKA.
Friday, February 8, 2013
Tanzia: Askofu Mstaafu Amedeus Msarikie wa Moshi, Afariki Dunia
![]() |
| Askofu Mstaafu Amedeus Msarikie |
Askofu mstaafu Amedeus Msarikie wa Jimbo Katoliki Moshi, Tanzania amefariki dunia Alhamisi, tarehe 7 Februari 2013 mjini Nairobi, Kenya alikokuwa akitibiwa saratani ya kibofu cha mkojo.
Kwa mujibu wa Radio Vatikani, habari za msiba zimethibitishwa na Askofu Isack Amani wa Jimbo Katoliki Moshi. Mipango ya maziko inaandaliwa na Jimbo, pia mazishi yatafanyika tarehe 14 February 2013.
Askofu Msarikie alizaliwa Kirua Vunjo Moshi, mwaka 1931. Alipewa daraja la Upadre tarehe 8 Agosti 1961 kama padre wa Jimbo la Moshi. Aliteuliwa na Baba Mtakatifu Yohani Paulo II kuwa askofu wa Jimbo la Moshi tarehere 21 Machi 1986. Alisimikwa rasmi kama askofu wa Jimbo la Moshi tarehe 1 Mei 1986 na Askofu Jozef Kadinali Tomko akisaidiwa na Makadinali Laurian Rugambwa na Maurice Michael Otunga.
Baada ya kulitumikia Kanisa la Moshi kwa miaka 26, Askofu Amedeus alistaafu kwa mujibu wa sheria ya Kanisa tarehe 21 Novemba 2007. Baada ya kustaafu, aliendelea kulihudumia kanisa kwa huduma mbali mbali za kiroho na kimwili. Jimbo la Moshi kwa sasa linaongozwa na Mh. Askofu Isaac Amani Massawe tangu Novemba 2007.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU
MAHALI PEMA PEPONI
AMINA
Subscribe to:
Posts (Atom)
