Thursday, January 17, 2013

MAOFISA WA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI WATEMBELEA TBL


 Baadhi ya maofisa kutoka Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) kutoka Dar es Salaam wakipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Uzalishaji Bia wa Kiwanda cha Bia cha TBL Arusha, Ben Mwanri (wa pili kushoto), walipotembelea Kiwanda cha Bia cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) cha Arusha, wakati wa  ziara ya siku moja kujionea shughuli mbalimbali za kiwanda hicho mwishoni mwa wiki.
 Baadhi ya maofisa kutoka Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) kutoka Dar es Salaam, wakiangalia eneo ambapo maji yaliyotumika kiwandani yanachujwa tayari kwa matumizi mengine, walipotembelea Kiwanda cha Bia cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) cha Arusha, wakati wa  ziara ya siku moja kujionea shughuli mbalimbali za kiwanda hicho mwishoni mwa wiki.

 Baadhi ya maofisa kutoka Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC), Usalama, wakitembelea mwishoni mwa wiki Kiwanda cha Bia cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), cha Arusha, walipofanya ziara ya siku moja kujionea shughuli mbalimbali za kiwanda hicho.
 Baadhi ya maofisa kutoka Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC), Usalama, wakitembelea mwishoni mwa wiki Kiwanda cha Bia cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), cha Arusha, walipofanya ziara ya siku moja kujionea shughuli mbalimbali za kiwanda hicho.
 Baadhi ya maofisa kutoka Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) kutoka Dar es Salaam wakipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Uzalishaji Bia wa Kiwanda cha Bia cha TBL Arusha, Ben Mwanri (wa pili kushoto), walipotembelea Kiwanda cha Bia cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) cha Arusha, wakati wa  ziara ya siku moja kujionea shughuli mbalimbali za kiwanda hicho mwishoni mwa wiki.
Kiongozi wa ujumbe wa maofisa wa Jeshi kutoka Chuo ChaTaifa cha  Ulinzi (NDC) Mafunzo ya Kijeshi na Usalama, S.M Minja  (kushoto) akimkabidhi zawadi  Meneja wa Uzalishaji Bia wa Kiwanda cha Bia cha TBL Arusha, Ben Mwanri, walipotembelea kiwanda hicho mwishoni mwa wiki.

Mshindi ‘Valentine Day’ kulamba Vitz

Meneja Mauzo na Masoko wa Push Media Mobile, Rodney Rugambo akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa shindano la kampeni maalum ya kuadhimisha sikukuu ya wapendanao ‘ Valentine Day’ iliyoandaliwa kwa kushirikiana na Kampuni ya African Media group (AMG) kupitia kituo cha televisheni cha Channel Ten na Redio Magic FM. Kushoto ni AFISA Masoko na Mauzo wa AMG,  Prosper Vedasto 




Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Push Media Mobile inatarajiwa kutoa zawadi ya gari aina ya Vitz lenye thamani ya sh milioni 8 kwa mshindi wa kampeni maalum ya kuadhimisha sikukuu ya wapendanao ‘Valentine Day’ inayoadhimishwa Februari 14 kila mwaka.

Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam Meneja Mauzo na Masoko wa Push Media Mobile, Rodney Rugambo, katika uzinduzi wa kampeni hiyo pamoja na Kampuni ya African Media Group (AMG), kupitia kituo cha televisheni cha Channel Ten na Redio Magic FM.

Rugambo alisema kuwa, wameamua kutoa zawadi hiyo kubwa ili kuwafanya wapendanao wengi kushiriki na kupata nafasi ya kushinda.

Alisema kuwa, ili kuingia katika droo ya shindano hilo, unatakiwa kutuma neno ‘Penzi’ kwenda namba 15678 na kujibu maswali mbalimbali yahusiyo masuala ya mapenzi na siku ya Valentine.

“Hii ni promosheni ya kwanza kubwa hapa nchini na mshindi kujishindia gari, lengo kubwa ni kutoa ufahamu kuhusiana na sikukuu ya wapendanao na vile vile kuwazawadia wadau wetu kwa kushiriki katika shughuli zao za ujenzi wa taifa,” alisema Rugambo.

Alisema kuwa, mbali ya zawadi hizo, washiriki wa promosheni hiyo pia watapata nafasi ya kujishindia kompyuta (Laptop), aina ya HP yenye thamani ya sh milioni 1.5, simu aina ya Blackberry Curve yenye thamani ya sh 500,000 na ‘Home Theatre’ ya thamani ya sh 400,000.

Kwa mujibu wa Rugambo, lengo lao kubwa ni kuifanya sikukuu ya wapendanao kuwa kubwa kama nyingine, kwani mapenzi ni kitu muhimu katika maisha ya kila siku.

Alisema kuwa, mipango yao ni kuwekeza katika sikukuu hiyo, ambayo jamii imeanza kuitilia mkazo japo si siku ya mapumziko kama sikukuu nyingine, ambako mwaka huu, wameweka bajeti ya sh milioni 30 ili kufanikisha zaoezi hilo.

ALICHOKISEMA NAY WA MITEGO KUHUSU NYIMBO YAKE YA NASEMA NAO



Na Elizabeth John
MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amesema wimbo wake wa ‘Nasema Nao’, ambao unafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio na runinga, ni hisia zake binafsi na wala hana bifu na mtu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Nay, alisema kuwa alifanikiwa kurekodi wimbo huo baada ya kufika studio na kukuta mapigo bila wimbo, na ndipo alipoamua kufanyia mazoezi kabla ya kuirekodi na kuisambaza.

 Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’
Nay, alisema hakukusudia kumsema mtu, licha ya baadhi ya maneno ya wimbo huo kuwa na majina ya wasanii na viongozi, lakini lengo lake ni kufikisha ujumbe kwa jamii na si vinginevyo.

“Mimi ndiye msanii wa kwanza wa muziki wa kizazi kipya kutaja watu kwenye nyimbo nikiwa na lengo la kufikisha ujumbe ninaoukusudia kwa jamii, na humu simaanishi chochote kibaya,” alisema Nay Wa Mitego.

Mkali huyo wa Bongo Fleva, alisema katika hilo, hana ‘bifu’ na mtu yeyote na hatarajii kusikia akiingia katika malumbano na wasanii waliotajwa katika wimbo huo ambao unafanya vizuri katika redio mbalimbali nchini.

Baadhi ya wasanii waliotajwa katika wimbo huo ni pamoja na Selemani Msindi ‘Afande Sele’,  Hamad Ally ‘Madee’, Chid Benzi na viongozi wengine wa kisiasa.

MZEE MALECELA, WAZIRI MKUU MSTAAFU SUMAYE NA JAJI MKUU MSTAAFU SAMATTA WATOA MAONI KATIBA MPYA LEO


Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao leo kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Tume Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na Mjumbe wa Tume Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim (katikati).
Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao leo kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Joseph Warioba.
Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akipata maelezo kuhusu Kitengo cha Utafiti cha Tume ya Mabadiliko ya Katiba kutoka kwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume Bw. Mohammed Hamad leo mara baada ya kutoa maoni yake kuhusu katiba Mpya. Kushoto ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Joseph Warioba. 
Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao leo kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na Mjumbe wa Tume Prof. Mwesiga Baregu.
Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akitoka nje ya ukumbi wa mikutano wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo mara baada ya kutoa maoni yake kuhusu katiba Mpya. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na kulia ni Mjumbe wa Tume Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim.

Tuesday, January 15, 2013

"NO INTENTION FOR THE ABOLISH OF WITHDRAWINGBENEFITS"


The Minister for Labour and Employment, Gaudensia Kabaka has assured mine workers that the government has no intention to abolish withdrawal benefits in February, this year.

Opening a two-day social security funds stakeholders’ meeting in Mwanza City , Ms Kabaka strongly dismissed rumours that withdrawal benefits would be abolished in February, this year.

“This workshop is held to clear the air on withdrawal benefits, Tanzanians must understand that the government does not intend to abolish withdrawal benefits,” said Ms Kabaka.

She, however, said the government was collecting views from stakeholders to enable social security funds become effective, beneficial and friendlier to all workers.

Minister Kabaka said that the government had already instructed the Social Security Regulatory Authority (SSRA) to withdraw its public notice on withdrawal benefit.

According to her, the government believes that it is important to remove from the law the section that denies members right to withdrawal benefits.

Since the rumours of abolishing withdrawal benefits hit mining sector a few months ago, over 400 workers from Lake Zone major gold mines had tabled resignation letters.

Thomas Sabaya, an official from Tanzania Mining and Construction Workers Union (Tamico) in Geita Gold mine, said over 300 workers had written to have their jobs terminated by the end of 2012.

By MOSES MATTHEW, Tanzania Daily News
The Minister for Labour and Employment, Gaudensia Kabaka has assured mine workers that the government has no intention to abolish withdrawal benefits in February, this year.

Opening a two-day social security funds stakeholders’ meeting in Mwanza City , Ms Kabaka strongly dismissed rumours that withdrawal benefits would be abolished in February, this year.
 
“This workshop is held to clear the air on withdrawal benefits, Tanzanians must understand that the government does not intend to abolish withdrawal benefits,” said Ms Kabaka.
 
She, however, said the government was collecting views from stakeholders to enable social security funds become effective, beneficial and friendlier to all workers.
 
Minister Kabaka said that the government had already instructed the Social Security Regulatory Authority (SSRA) to withdraw its public notice on withdrawal benefit.
 
According to her, the government believes that it is important to remove from the law the section that denies members right to withdrawal benefits.
 
Since the rumours of abolishing withdrawal benefits hit mining sector a few months ago, over 400 workers from Lake Zone major gold mines had tabled resignation letters.
 
Thomas Sabaya, an official from Tanzania Mining and Construction Workers Union (Tamico) in Geita Gold mine, said over 300 workers had written to have their jobs terminated by the end of 2012.
 
By MOSES MATTHEW, Tanzania Daily News

MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA ASEMA VIFO VYA MAMA NA WATOTO BADO NI CHANGAMOTO KWA AFRIKA


Makamu wa Rais Dr.Mohamed Gharib Bilal amesema Bara la Afrika bado linachangamoto kubwa katika kuweka sera na mipango itakayosaidia kupunguza vifo vya kina mama hususani katika kipindi cha ujauzito,wakati wa kujifungua na kuzuia vifo vya watoto walio chini ya umri wa 
miaka mitano

Makamu wa Rais ameyasema hayo Jijini Arusha wakati akifungua rasmi mkutano wa pili wa kimataifa unaowakutanisha wataalamu wa masuala ya afya kutoka nchi mbalimbali duniani wakiangazia namna ya kupunguza vifo kwa akinamama wajawazito,wanaojifungua na watoto walio na umri chini ya miaka mitano

Dr.Bilala mesema japokuwa nchi ya Tanzania kwa upande wake imekuwa ikijitahidi kupunguza idadi ya vifo vya watoto lakini takwimu zinaonesha idadi ya vifo vya kinamama bado ipo juu na hivyo ni lazima kuwepo na uwajibikaji katika kuokoa maisha ya akinamama na watoto

Kwa upande wake waziri wa Afya wa Tanzania Dr.Hussein Ally Mwimyi amesema tangu mwanzoni mwa miaka ya 1970 Tanzania imekuwa ikiendesha miradi mbalimbali inayohusu uboreshaji wa afya ya mama na mtoto hali iliyopelekea kwa hivi sasa huduma hizo kutolewa sii tu katika mahospitali bali pia katika vituo mbalimbali vya afya

Awali waratibu wa mkutano huo shirika la Management and development for health (MDH) kupitia kwa mkurugezi wake Dr.Chalamilla Guerino, ameeleza kuwa mkutano huo unatarajiwa kuleta majibu yatakayosaidia kuboresha kuduma na kuhakikisha mama hapotezi maisha wakati wa kuleta uhai.

Monday, January 14, 2013

MIRUNGI "GOMBA" YAKAMATWA ARUSHA


Jeshi la Polisi mkoani Arusha  limewakamata watu wanne wakiwa na madawa ya kulevya aina ya mirungi. Watu hao walikuwa na jumla ya viroba 202 vya dawa hizo  ambazo zilikuwa kwenye gari aina ya Mitsubishi Canter lenye namba za usajili T 306 BUN.
 
Akizungumza na waaandishi wa habari nje ya jengo la Makao Makuu ya Jeshi hilo Mkoani hapa, Kamanda wa Polisi Mkoani humo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Liberatus Sabas aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Joel Alfayo Lukumay (37), Rahim Azizi Gilla (35), Ibrahimu Solomon Katambwei (40) na Musa Lazaro Mollel (38) wote ni wakazi wa Mkoa wa Arusha.

Alisema tukio hilo lilitokea leo saa 1:00 asubuhi katika eneo la Engikareti lililopo wilayani Longido mkoani hapa. Aliongeza kwa kusema kwamba, mafanikio hayo yametokana na taarifa toka kwa raia wema ambao waliwasiliana na jeshi hilo, ambapo mara baada ya kupata taarifa hiyo waliweka mtego katika eneo hilo na kufanikiwa kulikamata gari hilo ambalo lilikuwa linatokea nchi jirani ya Kenya.

Kamanda Sabas aliwashukuru wananchi wa Mkoa wa Arusha kwa ushirikiano wao  mkubwa unaofanywa kwa jeshi hilo na kuwaomba waendelee kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwani kama wananchi wakiamua uhalifu unaweza ukapungua kwa kiasi kikubwa.

Baadhi ya waaandishi na askari waliokuwa kwenye eneo hilo walishuhudia viroba hivyo vikiwa na majina ya watu pamoja na uzito wa kila mzigo huku wengine wakidai kwamba inawezekana gari hilo huwa linabeba mizigo ya watu mbalimbali ambao wanakuja kugawana mara baada ya kuingia Arusha Mjini.

Kutokana na tukio hilo Jeshi la Polisi Mkoani hapa linaendelea kuwahoji watuhumiwa hao na pindi upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili. Aidha taarifa za ndani ya jeshi hilo zinasema kwamba gari hilo lilishawahi kukamatwa tarehe 16 mwezi Machi mwaka jana ambalo lilikutwa na madawa ya aina hiyo na kesi yake ilikwishafikishwa mahakamani na bado shauri hilo bado linaendelea.