Thursday, January 10, 2013

Shule za sekondari Singida zatakiwa kuwa na maabara tatu zilizokamilika kabla ya Novemba 2013.


 Mkuu wa wilaya ya Singida mwalimu Queen Mlozi (wa pili kushoto) akikagua ujenzi wa maabara tatu za shule ya sekondari kata ya Mitunduruni  jimbo la Singida mjini.Wa kwanza kushoto ni diwani wa kata ya Mitunduruni,Sorongai Pantaleo.
 Diwani wa kata ya Mitundurinu (CCM) jimbo la Singida mjini,Sorongai Pantaleo (wa kwanza kushoto) akizungumza na mkuu wa wilaya ya Singida mwalimu Queen Mlozi ofisini kwa mkuu wa shule ya sekondari kata ya Mitunduruni.
 Mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi, (wa pili kutoka kulia) akikagua ujenzi wa choo katika shule ya msingi ya Unkyankindi kata ya Mitunduruni.Wa kwanza kulia ni diwani wa kata ya Mitunduruni Bw.Sorongai Pantaleo.
Baadhi ya vyumba vya madarasa  vilivyojengwa na mbunge wa jimbo la Singida mjini,Mohammed Gullam Dewji.
  
Mkuu wa wilaya ya Singida Mwalimu Queen Mlozi amewahimiza wakuu wa shule za sekondari kuwa wabunifu katika kutafuta misaada na fedha kwa ajili ya kugharamia ujenzi  wa maabara.
Amesema kwa vile sio rahisi kwa serikali kufanya kila kitu ikiwemo kujenga kwa mpigo maabara katika shule zote za sekondari nchini, kuna umuhimu mkubwa kwa wananchi na wadau wengine kusaidiana na serikali.
Mkuu huyo wa wilaya ametoa changamoto hiyo wakati akizungumza na

Sunday, January 6, 2013

ZAMBIA WANYUKWA TENA 2-0



Mabingwa watetezi wa Kombe la Mataifa ya Afrika Zambia wamejikuta wakinyukwa tena mechi ya tatu mfululizo na timu ya taifa ya Angola ambayo watakutana kwenye michuano hiyo siku chache zijazo kwa mabao 2-0.

Mchezaji wa Angola anayechezea Klabu ya Daraja la Pili nchini Brazil katika klabu ya  Parana Geraldo alitupia bao la kuongoza katika dakika ya 8 ya mchezo huo uliochezwa katika uga wa Dobsonville na baada ya dakika 5 yaani dakika ya 13 ya mchezo Mlinzi Amaro anayechezea daraja la kwanza alizifumania nyavu na mabao hayo kudumu hadi dakika 90 za mchezo.

Zambia itaanza kampeni zake Januari 21 na timu ya Ethiopia  mechi itakayochezwa katika mji wa Nelspruit ulio Kaskazini Mashariki mwa Afrika Kusini.

Itakumbukwa kwamba Zmabia ilipoteza michezo yake miwili ilipokutana na Saudia na Taifa Stars.

Hata hivyo Zambia ina mechi 3 kabla ya kuingia katika michuano hiyo na Morocco, Norway na Namibia kwani katika AFCON ipo kundi C na Nigeria, Ethiopia nab U

UCHE KALU AJITOA SUPER EAGLES

Mshambuliaji wa Timu ya Nigeria na Klabu ya Rizespor Uche Kalu amejiondoa katika Kikosi cha Nigeria kilichopo Mjini Faro nchini Ureno kilipopiga kambi kwa ajili ya Michuano ya Soka ya Mataifa barani Afrika.

Kalu Uche Kalu Uche of Nigeria during the International Friendly match between France and Nigeria at the Stade Geoffroy-Guichard on June 2, 2009 in St Etienne, France.
Rizespor Uche Kalu
Mnigeria huyo amejiondoa katika kikosi hivyo kutokana na kusumbuliwa na nyonga. Itakumbukwa kwamba mchezaji huyo wa zamani wa Klabu ya Enyimba alipatwa na majerha hayo majuma machache yaliyopita lakini Daktari wa timu aliweza kumsaidia na kumpatia huduma ambayo ilimfanya aonekane nafuu. Pia Uche Kalu alikosa mechi ya Kirafiki siku Jumatano dhidi ya Catalonia.

Timu ya Taifa ya Nigeria inaongozwa na Kocha Stephen Keshi

NIGERIA YAAMUA KUACHANA NA AMEOBI



Shola Ameobi
Shirikisho la Soka la Nigeria limefunga muda wake wa kumtaka Shola Ameobi anayechezea klabu ya Newcastle kuthibitisha kama atakwenda na kikosi cha Timu ya Taifa hilo nchini Afrika Kusini katika michuano ya AFCON 2013.

Itakumbukwa kwamba jana katika michuano yaFA nchini Uingereza alitolewa kwa kadi nyekundu huku Newcastle wakitolewa katika mzunguko wa tatu wa michuano hiyo maarufu nchini Uingereza. Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 alicheza miezi miwili iliyopita na timu yake ya Taifa dhidi ya Venezuela  na kuonekana kuwa ana mchango kwenye timu ya taifa hilo. Shirikisho la Soka nchinihumo lilimpa muda wa kuthibitisha mpaka jana Jumamosi kama anaweza kuchezea timu hiyo ya Taifa katika AFCON hata hivyo hakuweza kuthibitisha kufanya hivyo, bila kutoa sababu yoyote ya msingi. 

Michuano ya Mataifa ya Afrika AFCON nchini Afrika Kusini kuanzia Januari 19 hadi Februari 10.

MKANDARASI ATAKIWA KUZOA TAKATAKA

Jalala likifanyiwa Usafi
 Baadhi ya wakazi wa Sanya juu wilyani Siha mkoani Kilimanjaro wametaka mkandarasi wa kuzoa taka katika maeneo ya Sanya mjini na mitaa yake kutoa huduma hiyo kila siku
 Wakazi hao wametoa malalamiko hayo kwa nyakati tofauti walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni. Wamesema mkandarasi huyo hivi sasa anazoa taka hizo kila baada ya wiki moja wakati mwingine hata zaidi na kusababisha mlundikano mkubwa wa taka zinazozagaa hovyo hadi kwenye makazi ya watu.

Mkazi moja amesema amechoshwa na kero ya harufu ya taka zinazozaga baada ya kutelekezwa, haswa sehemu yanapouzwa maembe kenye soko la sanya juu na sehemu ya mtaro wa kupitisha maji machafu ambapo umeota majani na mrundikano wa taka zinazotupwa na watu na kutishia kufukiwa kabisa kama hautafanyiwa usafi.

 Akijibu malalamiko hayo Bibi Afya wa Wilaya ya Siha Joys Temu amekiri kuwepo kwa taka hizo nakusema kuwa atalifanyia kazi jambo hilo kabla halijaleta hatari kwa wanachi wa maeneo hayo

KIKWETE ATUA SINGIDA KWA ZIARA YA SIKU 2



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitumia laptop yake kuwaonyesha viongozi mbali mbali wa Mkoa wa Singida wakati alipokuwa akiwaelezea masuala muhimu ya maendeleo nchini.Rais Kikwete amewasili Mjini Singida Januari 5 kwa Ziara ya kikazi ya Siku Mbili.

Picha na IKULU YA TANZANIA